NAFASI ZA KAZI : MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III - NAFASI 14
   Mkurugenzi  Mtendaji wa Halmshauri ya Wilaya ya Tabora Uyui anawatangazia nafasi za  kazi kwa wananchi wote wenye sifa za kuomba nafasi hizo kama  inavyoonyesha hapo chini   MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III - NAFASI 14   SIFA ZA MWOMBAJI   Awe  amehitimu elimu ya kidato cha Sita/Nne na Mafunzo ya Astashahada/cheti  katika moja ya fani zifuatazo: Utawala, Sheria, Elimu ya Jamii,  Usimamizi wa Fedha, Maendeleo ya Jamii na Sayansi ya sanaa kutoka Chuo  cha Serikali za Mitaa Hombolo Dodoma, au Chuo chochote kinachotambuliwa  na Serikali.   KAZI ZA KUFANYA  - Afisa Masuuli na Mtendaji Mkuu wa Serikali ya Kijiji.  - Kusimamia ulinzi na Usalama wa raia na mali zao.  - Kuratibu na kusimamia upangaji wa utekelezaji wa Mipango ya Maendeleo ya Kijiji.  - Katibu wa Mikutano na Kamati zote za Halmashauri ya Kijiji.  - Kutafsiri na kusimamia Sera, Sheria na Taratibu.  -  Kuandaa Taarifa za Utekelezaji wa kazi katika eneo lake na Kuhamasisha  wananchi katika kuandaa na kutekeleza mikakati ya kuond...