KUONGOZWA NA ROHO MTAKATIFU KATIKA KWELI YOTE
  NA MWL, AYOUB LEO   WIKI YA MAOMBI TAREHE 08,10,11,12,NA 12 JANUARI 2018,FPCT KISESA   Roho Mtakatifu ni nani ?   Ni Roho wa Mungu .Kwa nini anaitwa Roho wa  Mungu ?   Kwa sababu ni Mungu mwenye sifa za Ki-ungu.Sifa hizo ni :-   v   Anadumu milele Ebr 9 :14   v   Yupo kila mahali   v   Ni mwenye nguvu zote   v   Ana ufahamu wote   v   Anafufua   v   Anaumba   KAZI YA ROHO KATIKA KUONGOZA WATU  KWENYE KWELI YOTE   a)     Kuwapasha wana wa Mungu juu ya mambo yajayo Yoh 16 :13. Wanadamu hawana uwezo wa kujua yanayotokea mbeleni pasipo kuwa na msaada wa nguvu juu yao.Roho Mtakatifu ndiye awezaye kuwafunulia na kuwajulisha juu yale yatakayokuwepo.   b)     Kuwajulisha /kuwahakikishia wana wa Mungu juu ya urithi wao kwa Mungu .Roho Mtakatifu ndiye anayeweza kuwapa uhakika wa kile wanachorithi au watakachopokea kutoka kwa Mungu.Gal 4:6-7,Rum 8 :14-17   c)     Kuwaongoza wana wa Mungu katika kuishinda dhambi ...