WOKOVU NI KUWA NA USHIRIKA
  SEHEMU YA KWANZA  KWELI KUU:     Maisha  yetu ya wokovu hayana maana kabisa kama hatutakuwa na ushirika na Baba,  Mwana, Roho Mtakatifu, na sisi kwa sisi kama kanisa la Kristo ambalo ni  mwili wa Kristo.     Mstari wa Msingi (Kukumbuka):   1 Wakorintho 1:9    Mungu ni mwamainifu ambaye mliitwa na yeye mwingie  katika ushirika  wa Mwanawe , Yesu Kristo Bwana wetu.       Ndugu mpendwa, leo nitaanza mfululizo wa somo hili ambalo litakuwezesha  wewe kueneza mizizi yako ya imani katika Yesu Kristo Bwana wetu ambaye  ni Mungu Mwana, na katika Mungu Roho Mtakatifu na katika Mungu Baba kwa  kujua nini maana ya kuwa na ushirika, namna ya kuwa na ushirikana jinsi  ya kuendelea kuwa na ushirika Mungu (Baba, Mwana na Roho Matakatifu).  Karibu sana.    UTANGULIZI:  Katika utangulizi wetu, tutaangalia zaidi maana ya maneno makuu matatu  ambayo yatajitokeza katika somo letu hili na miongoni mwa maneno hayo  mawili yamejitokeza katika kichwa cha somo letu. Hivyo ni lazima  tuyaangalie ili tuwe na ...