NAMNA MWANAMKE ANAVYOWEZA KUTUMIA NAFASI ZAKE KUBADILISHA MAISHA YA NDOA YAKE (Sehemu ya 4a)
    Na: Patrick Sanga      Nafasi ya tano – Mwanamke kama Mjenzi   Katika sehemu ya tatu tuliangalia nafasi ya nne ambayo ni Mwanamke kama Mlinzi. Ili kuisoma endapo hukusoma bonyeza link hii https://nsanacz.blogspot.com/2018/05/namna-mwanamke-anavyoweza-kutumia_6.html. Fuatana nami sasa tuendelee na mfululizo wa somo hili.   Biblia katika kitabu cha Mithali 14:1 inasema ‘ Kila mwanamke aliye na hekima huijenga nyumba yake: Bali aliye mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe’. Tafsiri  ya neno nyumba ni familia, naam na familia inajumuisha baba, mama na  watoto endapo mmejaliwa. Hata hivyo katika hali ya kawaida watoto  watalelewa katika msingi mzuri endapo ndoa husika imetengamaa. Ifahamike  kwamba hili andiko si la wanandoa peke yao, bali hata wanawake wasio  wanandoa wenye familia kama wajane, walezi nk linawahusu. Kwa kuwa hapa  tunazungumzia habari za wanandoa nitalifafanua zaidi kutoka kwenye kona  hiyo. Pia neno nyumba limetumika ili kutupatia urahisi wa kuelewa namna  nyu...