MIKOPO YA ELIMU YA JUU
- Pata kiungo
 - X
 - Barua pepe
 - Programu Nyingine
 
Friday, November 3, 2017
Bodi ya mikopo Yawatoa Hofu Wanafunzi
Bodi
 ya Mikopo ya Elimu ya juu nchini (HESLB) imewatoa hofu wanafunzi 
waliokosa mikopo kwakuwa ipo katika hatua za mwisho kutoa majina ya 
awamu ya tatu.
Kauli
 hiyo imekuja ikiwa leo   ni siku ya mwisho iliyotolewa na Naibu Waziri 
wa Elimu, Sayansi na Teknolojia William Ole Nasha ya kuitaka bodi hiyo 
kuhakikisha kila mwanafunzi mwenye sifa anapewa mkopo.
Akizungumza
 leo Novemba 3,Meneja Mawasiliano wa bodi hiyo, Omega Ngole amesema 
agizo hilo linaendelea kutekelezwa na kwamba hadi kufikia kesho  kila 
mwanafunzi mwenye sifa atapata mkopo.
Amesema kwa wale watakaokosa mkopo wanaweza kukata rufaa kupitia bodi hiyo ili kupitia upya taarifa zao.
“Maelekezo hayo yote yanatekelezwa na tutakamilisha leo na tutatoa taarifa ya kuhusu utekelezaji wake wiki ijayo,” amesema
Katika
 mwaka wa masomo wa 2017/18 Serikali imetenga bajeti ya Sh427 bilioni 
kwaajili ya mikopo ambapo wanafunzi 30,000 wa mwaka wa kwanza 
watanufaika na fungu hilo.
Hadi
 sasa Jumla ya wanafunzi 21,677 maombi yao yamekubaliwa ikiwa ni awamu 
mbili zilizotolewa na bodi hiyo ambapo awamu ya kwanza ilitoa majina 
10,196 na ya pili 11,481.
Meneja
 huyo amesema kwa wale waliodahiliwa kwenye vyuo walivyothibitisha 
kupitia Tume ya Vyuo Vikuu (TCU) tayari fedha zimeanza kutumwa kwenye 
vyuo husika.
“Mwanafunzi
 akipangiwa mkopo halafu asipoliridhika, akaona uhitaji wake ni mkubwa 
kuliko kiwango alichokipata kuna nafasi ya kukata rufaa ambayo itaanza 
wiki ijayo,”amesema.
M
- Pata kiungo
 - X
 - Barua pepe
 - Programu Nyingine
 

Maoni