Machapisho
Inaonyesha machapisho kuanzia Mei, 2018
NAMNA MWANAMKE ANAVYOWEZA KUTUMIA NAFASI ZAKE KUBADILISHA MAISHA YA NDOA YAKE
- Pata kiungo
 - X
 - Barua pepe
 - Programu Nyingine
 
 SEHEMU YA NNE B  Na: Patrick Sanga     Nafasi ya tano – Mwanamke kama Mjenzi   Katika sehemu ya 4a tulianza kwa kuangalia nafasi ya tano hata hivyo  kutokana na urefu wake nikaona vema kuigawanya nafasi hii ya tano katika  kipengelea a na b. Ili kusoma sehemu ya 4a bonyeza link ifuatayo  https://nsanacz.blogspot.com/2018/05/namna-mwanamke-anavyoweza-kutumia_47.html Katika sehemu ya 4b tutangalia ni kwa namna gani mwanamke atapata  hekima ya kumsaidia kujenga ndoa yake. Karibu sasa tuendelee…   Hebu tuanze kwa kuangalia mstari wa ajabu sana katika Muhubiri 7: 12 unasema ‘Kwa maana hekima ni ulinzi, kama vile fedha ilivyo ulinzi, na ubora wa maarifa ni ya kwamba hekima humhifadhi yeye aliyonayo’ .  Hekima ndio nguzo kuu ya ujenzi wa ndoa yako, naam ukiwa nayo ni  dhahiri kwamba italeta uponyaji kwenye ndoa yako pia. Mwanamke kama  mjenzi anahitaji kuwa na hekima ili kulinda ndoa yake akijua kwamba ki –  nafasi yeye ni Mlinzi wa mumewe. Kumbuka kwamba andiko letu la msingi  katika se...
NAMNA MWANAMKE ANAVYOWEZA KUTUMIA NAFASI ZAKE KUBADILISHA MAISHA YA NDOA YAKE (Sehemu ya 4a)
- Pata kiungo
 - X
 - Barua pepe
 - Programu Nyingine
 
    Na: Patrick Sanga      Nafasi ya tano – Mwanamke kama Mjenzi   Katika sehemu ya tatu tuliangalia nafasi ya nne ambayo ni Mwanamke kama Mlinzi. Ili kuisoma endapo hukusoma bonyeza link hii https://nsanacz.blogspot.com/2018/05/namna-mwanamke-anavyoweza-kutumia_6.html. Fuatana nami sasa tuendelee na mfululizo wa somo hili.   Biblia katika kitabu cha Mithali 14:1 inasema ‘ Kila mwanamke aliye na hekima huijenga nyumba yake: Bali aliye mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe’. Tafsiri  ya neno nyumba ni familia, naam na familia inajumuisha baba, mama na  watoto endapo mmejaliwa. Hata hivyo katika hali ya kawaida watoto  watalelewa katika msingi mzuri endapo ndoa husika imetengamaa. Ifahamike  kwamba hili andiko si la wanandoa peke yao, bali hata wanawake wasio  wanandoa wenye familia kama wajane, walezi nk linawahusu. Kwa kuwa hapa  tunazungumzia habari za wanandoa nitalifafanua zaidi kutoka kwenye kona  hiyo. Pia neno nyumba limetumika ili kutupatia urahisi wa kuelewa namna  nyu...
NAMNA MWANAMKE ANAVYOWEZA KUTUMIA NAFASI ZAKE KUBADILISHA MAISHA YA NDOA YAKE (Sehemu ya 3)
- Pata kiungo
 - X
 - Barua pepe
 - Programu Nyingine
 
      Na: Patrick Sanga   Nafasi ya nne – Mwanamke kama Mlinzi     Katika sehemu ya pili tuliangalia nafasi tatu za awali ambazo ni nafasi ya Msaidizi, Mshauri na Mleta kibali . Ili  kusoma sehemu ya pili bonyeza link hii  https://nsanacz.blogspot.com/2018/05/namna-mwanamke-anavyoweza-kutumia_4.html .Kumbuka  kwamba lengo la ujumbe ni kuangalia ni kwa namna gani Mwanamke  aliyeolewa anaweza kutumia nafasi zake kubadilisha/kuiponya ndoa yake.  Katika sehemu hii ya tatu tutaangalia nafasi ya mwanamke kama Mlinzi.  Naam kwa rejea kumbuka kwamba, msingi wa somo hili ni maneno ambayo  Octoba 2009 BWANA aliniambia akisema ‘ Waambie wanawake wasimame kwenye nafasi zao ndipo wataona uponyaji kwenye ndoa zao’ .    Labda nianze kwa kuuliza, je una fahamu kwamba wajibu wa kumlinda mumeo ni wako? Naam Mungu amejiwekea utaratibu mpya kwamba Mwanamke amlinde mwanaume.   Je ni ulinzi wa namna gani? Ni ulinzi wa kiroho ndio ambao mwanaume  anahitaji kutoka kwa mkewe. Mke anatakiwa kuwa makini...
NAMNA MWANAMKE ANAVYOWEZA KUTUMIA NAFASI ZAKE KUBADILISHA MAISHA YA NDOA YAKE (Part 2)
- Pata kiungo
 - X
 - Barua pepe
 - Programu Nyingine
 
      Na: Patrick Sanga   Maada:  Nafasi ya Msaidizi, Mshauri na Mleta kibali       Ili kusoma sehemu ya kwanza bonyeza link hii https://nsanacz.blogspot.com/2018/05/namna-mwanamke-anavyoweza-kutumia.html     Mpenzi msomaji, Mungu akubariki kwa kufuatilia mfululizo wa somo  hili. Ni imani na maombi yangu kwamba masomo haya yatafanyika msaada  kwenye maisha yako na ndoa yako kwa ujumla. Katika sehemu hii ya pili  nitaandika kuhusu nafasi tatu ambazo ni nafasi ya Mwanamke kama Msaidizi, Mshauri na Mleta kibali.     Mwanamke kama Msaidizi     Mwanzo 2:18 ‘ BWANA Mungu akasema, Si vema huyo mtu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye’ .  Ukisoma mstari huu katika toleo la GNB Biblia inasema ‘ Then the LORD God said, “It is not good for the man to live alone. I will make a suitable companion to help him. ”  Biblia inatueleza kwamba Adam ndiye aliyetangulia kwanza kudhihirishwa  kabla ya Mwanamke. Kabla ya Hawa kuletwa, Mungu alimpa Adam majukumu  mengi ambayo alip...
NAMNA MWANAMKE ANAVYOWEZA KUTUMIA NAFASI ZAKE KUBADILISHA MAISHA YA NDOA YAKE
- Pata kiungo
 - X
 - Barua pepe
 - Programu Nyingine
 
      Na: Patrick Sanga   Mithali 14: 1 ‘Kila mwanamke aliye na hekima hujenga nyumba yake; Bali aliye mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe’ .   Mchungaji mmoja rafiki yangu aliniambia asilimia hamsini mpaka sabini  ya changamoto au matatizo anayoshughulika nayo mara kwa mara katika  kanisa lake ni ya wanandoa. Kwa lugha nyepesi asilimia 50 – 70 ni  matatizo yatokanayo au yanayohusiana na ndoa. Binafsi pia kwa upande  wangu kupitia nafasi yangu katika mwili wa Kristo, email za wasomaji  ninazopata na pia baadhi ya semina za ndoa ambazo nimefanya kuhusu eneo  hili nimegundua kwa hakika ndoa nyingi za wana wa Mungu zina shida na  wao hawajajua kwamba vita hii inatoka kwa Shetani, maana anajua ndoa  zikitengamaa ni faida kwa ufalme wa Mungu na ni uharibifu kwenye ufalme  wake wa giza. Naam anapigana usiku na mchana ili kuhakikisha ndoa  hazitengamai kwa kuleta fujo za kila aina.   Kila siku katika ndoa kuna changamoto zinazaliwa mpaka imefika mahala  baadhi ya wanandoa wanawaza kwa ...